View all from Eric Wainaina
Enable Javascript and Adobe Flash player in your browser to browse the full media gallerySawa sawaEric WainainaSwahiliEric Wainaina2005
Mzee alisema hakuna cha bure
Huo msema tumeutafsiri kinyume
Hata shule kuiingiza mtoto
Lazima utoe mchoto
Kupata simu ni balaa
Road license bei nafuu utanunua
Kupoteza ID ni mashaka
Twaarudisha Jamhuri yetu nyuma
Nchi ya kitu kidogo![]()
ni nchi ya watu wadogo
Ukitaka chai ewe ndugu nenda Limuru
Hata nyumbani ukipatwa na majambazi
Kupiga 999 wasema, 'Sisi hatuna gari
Lete elfu tano ya petroli, saidia utumishi'
Mahakamani hela ndio haki
Kwa elfu chache mshtakiwa ndiwe mshtaki
Ushahidi hwa utajiri
Twarudisha Jamhuri yetu nyuma jamani
Nchi ya kitu kidogo
ni nchi ya watu wadogo
Ukitaka soda ewe Inspekta burudika na Fanta
Nchi ya kitu kidogo
ni nchi ya watu wadogo
Ukitaka chai ewe Mama nunua Ketepa
Huko Kenyatta madawa zimeisha
Mashiti zauzwa marikiti mia kwa mia
Wafanyi kazi waenda miezi bil pesa
Ni bahati ukitibiwa
Mzigo wetu nazidi kuwa mzito
Watoto wanne na mshahara wa elfu mbili mia tano
Ya viatu, ya vitabu na vyakula
Nauliza na Mbotela
'Je, huu ni ungwana?'
Nchi ya kitu kidogo
Ni nchi ya watu wadogo
Ukitaka chai ewe ndugu nenda Limuru
© Eric Wainaina













Eric Wainaina is one of my favorite musicians and a true son of Kenya. He is a patriot and I hope his music sends him places, like winning Grammys, etc. He should keep it up and stay with his positive music.
Poster un nouveau commentaire